top of page

NENO LA MUNGU KWA LAODIKIA

Nalimwona mpenzi wangu, limbuko la ujana wangu. toka mbali nalimwita lakini asiitike, nikasema huenda amekuwa kiziwi nilipokuwa safari ya mbali. Nikampungia mkono apate kuniona, na kumbe ni kipofu! Nikajitia nguvu kumfuatia nipate kumrudisha, naam , nikamfikia. Na kumbe ni uchi, mavazi yake niliyompatia siku za uchumba alikuwa nayo yamechakaa, yasiweze kumsitiri uchi wake, naam ni kitanda cha buibui. 

​

Nikamsemesha, mavazi na dawa ya kujipata macho yako upate kuona yapo mikononi mwangu. Naye akasema ni nani wewe? nikasema, mimi ndiye uliyeapa apa tangu ujana wako kuwa utanipenda daima, naam, nimekuja nikutwae hata nyumba ya Baba yangu. Mpenzi wangu akasema, tazama mimi sasa ni mtu mzima, nasema kama mtu mzima na wala si kijana tena, Nalikuwa masikini sasa ni tajiri, naam, ni kitu gani utanipa nisichokuwa nacho hata niambatane nawe?

​

Ijapokuwa mpenzi wangu alikuwa uchi alijiona kuwa tajiri, ijapokuwa alikuwa kipofu hakutwaa dawa ya macho mikononi mwangu. Mwenye masikio na asikie!

MJUE MUNGU NA KRISTO WAKE UPATE UZIMA

3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

                    Yohana 17:3

Recent Posts

Our Mission of Faith

Our Purpose

Injili Ya Yesu Jioni is dedicated to spreading the teachings of Jesus through engaging content. We aim to inspire faith and foster a community where believers connect and grow spiritually. Join us as we explore the richness of God's Word together.

bottom of page